Pages

Friday, July 25, 2014

Matokeo ya kidato cha nne na changamoto zake

Unajua maana ya BIG RESULTS NOW?? Fuatilia matokeo haya ya kidato cha sita.

Division zero mwaka jana 2604, mwaka huu 612. Tofauti watu 1992, sawa na asilimia 325%.

Division one, mwaka jana 325, mwaka huu 4,365. Tofauti 4040, sawa na asilimia 1243%. Haya ni maajabu ya karne.

Walitanua ukubwa wa goli ili iwe rahisi kufunga... Kutoka zero zaidi ya 2000 mwaka jana hadi zero 600 tu mwaka huu. Kutoka div.one 300 tu mwaka jana hadi one zaidi ya 4,000 mwaka huu.

Hivi waalimu walewale wa shule zilezile zilizotoa one 300 mwaka jana ndo wametoa one 4,000 mwaka huu??

Changamoto zao zimetatuliwa? Maabara zimejengwa? Vitabu vimeongezwa? Madai ya walimu yamelipwa? Waalimu wa Kiswahili wameacha kufundisha Hesabu kutokana na ukosefu wa waalimu wa hesabu?

Kama changamoto hizo zote hazijatatuliwa mabadiliko haya ya ghafla kutoka div.one 300 hadi div.one zaidi ya 4,000 yametoka wapi? Kweli tumeamua kutanua goli tufunge kirahisi. Karibu Tanzania, hii ndiyo BRN bhana.!

Wanasema BRN means Big Results Now, mimi namwambia Waziri Kawambwa BRN, yani he should "Better Resign Now" maana watoto wetu wanapata BRN = Brain Receive Nothing.!!

Haya tia neno
Ndugu zangu wenye ndugu zao wenye ufaulu wa kuanzia D tatu form four na principle mbili kwa A level bado mnakaribishwa kwa kozi za uhasibu' manunuzi; masoko ; rasilimali watu na usimamizi wa biashara katika chuo chetu cha Tanzania Institute of Accountancy tembelea www.tia.ac.tz kwa maelezo zaidi

Sunday, May 6, 2012

Meru land crisis takes deadly turn

Meru land crisis takes deadly turn


IGP forms probe team



By Happy Lazaro and Staff reporter



Invasion of large scale farms in Meru took a deadly turn last Saturday when a villagers attempt to seize a large scale farm left one person dead and several injured.



Villagers from Poli and Seela Sing’isi in Meru district invaded Mito Miwili Farm owned by Pulses and Agro Commodities Company but armed guards fought them off leaving one person Noel Godson (32) from Sing’isi Ward dead after being shot. Another person Godlove Laeli (24) also suffered gunshot wounds and he is admitted at the Mount Meru regional hospital.



Arusha’s Regional Police Commander Thobias Andengenye confirmed the incident which happened on the night of April 28 adding that the about 40 invaders armed with bows and arrows, bush knives, double edged simes, spears and axes destroyed several items in the farm.





A wave of farm invasions has hit Arumeru district where there are about 20 large scale farms

owned by investors. Above villagers of Maroroni and Maji ya Chai listening to Arusha Regional

Commissioner Magessa Mulongo (not in the photo) who last week urged them to

stop the criminal actions. (Photo by Filbert Rweyemamu)







They set fire on four tractors and a storage house that had fertilizers and an assortment of seeds. As they wrecked havoc to the properties, they also stole whatever they could lay their hands on. By the time we went to press the value of the property that had been destroyed or stolen had not been



Mito Miwili farm invasion by villagers is the third in less than one month. In recent days Dolly Estate in Maji ya Chai saw its gate and part of an electric fence ripped apart by hordes of neighbouring villagers claiming that land belonged to them. Also on April 22 armed villagers of Nduruma, Nkoanrua and Akheri invaded a farm belonging to Machumba Estate and attempted to divide it among themselves. The process was stopped by riot Police.



The invasions are blamed on political parties’ politicians who during their Parliamentary campaigns during the by-elections in April this year promised land to the landless, apparently eyeing large estates within Meru district.

Meanwhile, The Inspector General of Police, Mr Said Mwema has commissioned a special team to pitch camp in Meru District, investigating the ongoing wave of estate invasions .



The delegation, led by the assistant commissioner of police, Mr Issaya Mngulu has already started work in Meru in association with the Regional Security Committee. However Mr Mngulu did not devulge how many people will be forming his team.



After the recent polls in Arumeru-East constituency in Meru District, irate villagers have been breaking into large scale farms in the vicinity claiming that they were promised during the preceding campaigns that they would be given land.



“We are going to stay here indefinitely,” said Mr Mngulu, explaining that there is no limit to the number of days that the team is required to accomplish the task but will only leave once the problem has been solved.





Assistant Commissioner of Police who is in the team, Mr Engelbert Mkoko stated here that theirs will be a professional undertaking which is going to leave no stone unturned.



“There are speculations that the farms invasion are being incited by politicians but our team will decide if that is the case or there are other deep rooted motives,” said the Police officer.



Meru District has a total of 20 large estates belonging mostly foreign investors.



“Our investigations will go hand-in-hand with mass education, teaching and advising local residents in Meru not to take seriously all politics or politicians that drive them into riots and other acts of peace breaching,” said Mr Mkoko.



The IGP team comes into Arusha just a week after the Regional Commissioner formed his own investigating committee to work on the Meru farm invasions.

Chadema waisambaratisha ccm Arusha

MBOWE ASEMA MAWAZIRI 7,WABUNGE 70 WAOMBA KUJIUNGA,10,000 WAKABIDHIWA KADI ARUSHA


Peter Saramba, Arusha

MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema kuna zaidi ya wabunge 70 kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameomba kujiunga na chama hicho cha upinzani.



Akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya NMC, Unga Ltd, jijini Arusha jana, Mbowe alisema katika orodha hiyo, wamo mawaziri saba waliotajwa katika Baraza lililotangazwa juzi na Rais

Jakaya Kikwete.



“Sasa wanaowataja akina Ole Millya, Bananga na wengine watashangaa kusikia orodha na majina ya wana CCM watakaojiunga Chadema,” alisema Mbowe.



Alitumia mkutano huo kuwatoa hofu wana Chadema wanaotilia shaka wimbi la viongozi na wana CCM wanaojiengua na kujiunga na chama hicho kikuu cha upinzani kuwa Chadema iko imara na hakiwezi kuhujumiwa wala kupenyezewa mamluki kama baadhi wanavyodhani.



Mbowe alitamba kuwa ameongoza harakati za upinzani kwa zaidi ya miaka

20 sasa ambayo imeanza kuzaa matunda kwa Watanzania kukiamini Chadema hivyo hawezi kukubali kuruhusu mtu yeyote yule anayetumia njia ya wazi au ya kificho kukidhoofisha.



“Kuna watu walipata hofu na kunitumia hadi sms kuhoji iwapo akina Ole Millya wametumwa na Lowasa (Edward Lowasa, Mbunge wa Monduli) kuja kukipeleleza Chadema, najua baadhi mko hapa na ninawatoa hofu kuwa

chama chetu ni taasisi imara isiyoweza kuhujumiwa na mtu au kundi la watu kwa nguvu wala mbinu yoyote,” alitamba Mbowe.



Aliwataka wanaofikiri Lowassa na wengine wenye ukwasi kuweza kununua viongozi wa Chadema kujiuliza kwanini hawakuweza kufanya hivyo kipindi chote walichokitumia kukijenga chama hicho ambacho ni tishio kwa CCMna mafisadi wote nchini.



Mbowe alitumia fursa hiyo kuponda uteuzi wa Baraza la Mawaziri akisema Rais Kikwete amevunja katiba kwa kuwateua watu ambao hawajaapishwa kuwa wabunge kushika nafasi za uwaziri.



Licha ya kuvunja katiba kwenye uteuzi, Rais pia amekiuka kwa kuwateua Wazanzibari kwenye wizara ambazo siyo za Muungano kama Afya aliyokabidhiwa na Dk Husein Mwinyi.





Makada wapokewa



Waliokuwa makada wa CCM waliojiengua na kuhamia Chadema walipokelewa na wote kuahidi kutumia uzoefu, juhudi na maarifa yao kisiasa kukijenga chama chao kipya kwa kushirikiana na wanachama na viongozi

wote.



Ole Millya aliahidi kudhihirisha kuwa hakua mzigo CCM kama wanavyodai baadhi ya viongozi mara alipotangaza kujiunga upinzani kwa kukifanyia chama hicho kitu ambacho hakitasahaulika milele akianzia na kuipenyeza

Chadema kwa jamii ya Wamaasai.



“Vijana wengi walioko ndani ya CCM wanaishi kwa matumaini ya kupewa vyeo kama ukuu wa wilaya na nyadhifa mbalimbali badala ya kusimamia haki na ustawi wa taifa,” alisema Ole Millya



Mila na laana kwa Ole Millya akigeuka



Kabla ya viongozi kuanza kuhutubia, wazee wa kimila wa jamii ya Wamaasai waliendesha sala ya Mila hiyo kwa kumkalisha kwenye kigoda Ole Millya na kumpa laani iwapo atageuka na kukisaliti Chadema.



“Mungu amekutuma wewe Ole Millya kuwakomboa Wamasaai kutoka kwenye utumwa waliokaa nao kwa miaka 50 kama ambavyo alimtuma Mussa kuwakomboa Waisraeli kutoka kwenye utumwa wa miaka 40 Misri. Usiwe

kinyonga kwa kugeuka, angalia huu umati ulioko mbele yako,” alisema Mzee Naftali Mollel



Kwa upande wao aliyekuwa Diwani wa Kata ya Sombetini, Alphonce Mawazo na Ally Banganga aliyekuwa mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM waliojiunga Chadema walisema chama hicho tawala tayari imekufa na kinasubiri kuepelekwa chumba cha kuhifadhia maiti kusubiri mazishi.



“Wanaohoji kwanini tumetoka CCM kwanza watueleze hicho chama kilipo kwa sababu tayari kimekufa mioyoni mwa wa Watazanania,” alisema Mawazo huku akishangiliwa



Akihutubia mkutano huo uliohudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema aliwataka wanaCCM wanaotaka kukihama chama hicho na kujiunga Chadema kufanya haraka kwa

sababu mlango wa ‘neema’ unakaribia kufungwa.



“Kuna kipindi kinakuja siku siyo nyingi ambapo kujiunga Chadema itakuwa dili. Wanaotaka kuja na wafanye hivyo sasa kabla hatujafunga milango,” alisema Lema



Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, alisema moto uliowashwa na Operesheni ‘Vua gamba, vaa gwanda’ ulioanzia Arusha, sasa umeanza kuenea nchi nzima akitaja matukio ya madiwani na wanachama

kadhaa kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa kuhamia Chadema.



Golugwa alisema baada ya mkutano wa jana Jijini Arusha, mikutano ya Operesheni ya Movement for Change inahamia wilaya za Longido, Ngorongoro, Simanjiro na kumalizikia Monduli.



Katika mkutano huo, Mbowe alikabidhi kadi za uanachama kwa Ole Millya, Bananga, Mawazo na viongozi kadhaa wana CCM waliojiunga Chadema ambapo kwa niaba ya wenzao.



Hamasa kubwa iligubika umati uliohudhuria baada ya mwana CCM mwenye asili ya kiasia aliyejitambulisha kwa jina la Adil Dewji alipopanda jukwani kurejesha kadi ya CCM na kujiunga Chadema.



Wengine waliojiunga Chadema kutoka CCM ni pamoja na wenyeviti kadhaa wa Serikali za mitaa kutoka Wilaya za Arusha, Monduli, Arumeru, Ngorongoro na Longido ambao waliwakilishwa na Ignas Mfinanga aliyekuwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Themi, jijini Arusha.



Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Friday, January 20, 2012

Tanzania

Mungu ailaze pahala pema peponi Mh. Jeremiah Sumari.
mwingine afariki Send to a friend


Thursday, 19 January 2012 20:51

0diggs

digg

NI JEREMIAH SUMARI WA CCM KUAGWA KESHO KARIMJEE

Fredy Azzah na Patricia Kimelemeta

SIMANZI nyingine imelikumba Bunge la Tanzania, kufuatia kifo cha Mbunge wa Arumeru Mashariki (CCM), Jeremiah Solomon Sumari (60),aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa muda mrefu akipatiwa matibabu.



Kifo cha Sumari kimetokea siku moja tu, tangu kufanyika kwa mazishi ya Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Regia Mtema aliyefariki dunia kwa ajali ya gari, Jumamosi iliyopita katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.



Sumari alianza kuugua kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, hali ambayo ilimfanya aende kampeni katika mazingira magumu.



Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtoto wa kwanza wa marehemu, Sioi Sumari alisema baba yake alipatwa na mauti katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alipokuwa amelazwa.



“Baba amefariki saa 8.30 usiku katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu,” alisema Sioi.

Alifafanua kuwa, marehemu anatarajiwa kuzikwa Jumatatu ijayo kijijini kwake katika jimbo la Arumeru Mashariki.

Mtoto huyo wa marehemu alisema baba yake utaagwa kesho (Jumamosi ) jijini Dar es Salaam, kabla ya kusafirishwa kwenda Arusha.



Ofisi ya Bunge Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema ofisi ya Bunge imepokea kwa masikitiko msiba huo kwani umetokea muda mfupi tangu waliporejea kutoka kwenye maziko ya Mtema.Hata hivyo, alisema kutokana na hali hiyo shughuli za Bunge zitaendelea kama zilivyopangwa na kwamba, zitasimamishwa siku ya kuaga mwili wa marehemu.



“Leo (jana) na kesho tutaendelea na shughuli za bunge kama kawaida, lakini siku ya kuaga tutasitisha shughuli ili kutoa fursa kwa wabunge kushiriki kwenye mazishi ya marehemu Sumari,” alisema Dk Kashililah. Alisema kwa sasa wanafanya taratibu za mazishi ya marehemu kwa kushirikiana na familia yake.



Alifafanua kwamba kutokana na hali hiyo, bunge limepata pigo kubwa baada ya kuondokewa na wabunge wawili katika kipindi kimoja, jambo ambalo limesababisha wabunge kushikwa na butwaa.Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema Kamati ya Uongozi ya Bunge itakutana leo kujadili namna ya kuratibu mazishi ya mbunge huyo.



Alisema kuna uwezekano mbunge huyo akaagwa katika ukumbi wa Karimjee, kama ilivyofanyika kwa mbunge wa Chadema Regia Mtema.



“Tunasikitika sana kwa kuwapoteza wabunge wawili ndani ya muda mfupi,” alisema Ndugai.



Kikwete amlilia

Kwa upande wake, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge, Anne Makinda kutokana na kifo cha Sumari.



Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Rais Kikwete ikisema; “Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa za kifo cha Mheshimiwa Jeremia Solomon Sumari….”

“Alikuwa kiongozi aliyewatumikia vema wananchi wa Jimbo lake la Uchaguzi la Arumeru Mashariki na Taifa kwa ujumla katika wadhifa wake wa Waziri kwa umahiri na uhodari mkubwa.”



Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Kikwete alisema kutokana na kifo cha Sumari, wananchi wa Arumeru Mashariki wamepoteza kiongozi wa kutegemewa. “Kwa moyo dhati, natuma salamu za rambirambi na pole kwa familia ya marehemu Jeremia Sumari kwa kumpoteza kiongozi na mhimili madhubuti wa familia,” taarifa hiyo ilimnukuu Rais Kikwete. Alifafanua akisema; “Ninawahakikishia kwamba nipo pamoja nanyi katika kuomboleza msiba huu mkubwa na namuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema aipumzishe roho ya marehemu Jeremia Solomon Sumari mahali pema peponi, Amina.”



Lowassa amlilia

Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa alisema taifa limepata pigo kubwa kwa kuondokewa na Sumari.

“Alikuwa mchapakazi sana.., hii imesababisha kuteuliwa kuwa Naibu Waziri katika serikali ya awamu ya nne, kutokana na umahiri wake,” alisema Lowassa.

Lowassa aliongeza kwamba, kutokana na hali hiyo, wananchi wa Arumeru Mashariki wamekosa mwakilishi wa kutetea maslahi yao bungeni.



Historia yake

Sumari alizaliwa Machi 2 mwaka 1943, katika kijiji cha Akeri wilayani Arumeru mkoani arusha.

Alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Meru Magharibi kati ya mwaka 1950 na 1957. Kati ya mwaka 1958- 1964 alisoma katika shule ya sekondari ya Old Moshi, mkoani Kilimanjaro na baadaye aliendelea na elimu ya juu nchini Uingereza.



Taarifa zinaonyesha kuwa, Sumari alipata elimu ya masoko kwa ngazi ya cheti ACCA, CIS, (Certificatein Marketing and Lincesed Broker lr), nchini Uingereza na baadaye kupata CPA nchini.

Kwa upande wa utumishi wake, mwaka 1996 mpaka 2004 alikuwa Mkurugenzi wa Bodi ya Boko la Disa Dar es Salaam (DSE).

Kisiasa , kuanzia mwaka 2005 mpaka mauti yalipomkuta alikuwa Mbunge wa jimbo hilo la Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CCM.



Januari 4 mwaka 2006, aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana na mwaka 2008 mpaka 2010 alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi.

source: mwananchi communication ltd

Friday, November 18, 2011

Katiba

Leo ni siku ya kusuka au kunyoa katika hatua ya kupata katiba mpya