Pages

Tuesday, March 22, 2011

Serikali yasitisha wagonjwa kupelekwa Loliondo

Tuesday, 22 March 2011 20:42

 Mussa Juma, Arusha na Dotto Kahindi

SERIKALI imewataka watu wanaowapeleka wagonjwa kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapile kupata tiba ya magonjwa sugu kuacha kufanya hivyo kwa muda kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kuharibu barabara ya kwenda Loliondo.



Imesema kwamba kuendelea kuongezeka kwa watu wanaokwenda huko wakiwa wagonjwa kutasababisha vifo kwa sababu magari mengi yanakwama barabarani maeneo ambayo hakuna huduma za vyakula, maji na dawa.



Kutokana na uamuzi huo na hali halisi ya barabara ya kufika huko, baadhi ya wananchi wamemwomba mchungaji huyo kuhamia jijini Arusha ili kuepusha madhara ambayo yanawakabili watu wanaohitaji huduma yake.



Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdore Shirima alisema Serikali haina nia ya kuwazuia watu kwenda kupata matibabu lakini mazingira yaliyopo sasa kuelekea katika Kijiji cha Samunge aliko Mchungaji Mwasapile, si mazuri.



"Naomba watu watuelewe, Serikali haina mpango wa kuwazuia kwenda kupata matibabu kwani suala hili ni la kiimani, lakini tunaomba watuelewe kuwa sasa hali si nzuri (kijijini) Samunge," alisema Shirima.



Alisema haitakuwa rahisi watu wanaokwenda sasa Samunge kupata huduma muhimu kama chakula, vinywaji na mahitaji mengine na wakati mwingine itawabidi kutembea kwa miguu kilomita 20 ili kufikia huduma hiyo.



Alisema katika kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa, ofisi yake imewasiliana na mikoa ya jirani ili watu wapewe elimu zaidi kuepuka athari zinazoweza kuwapata... "Sasa hali si nzuri. Tunaomba watuamini na hali ikiwa nafuu hasa kutokana na foleni ya magari, tutatoa taarifa."



Alisema Serikali inatarajia kukutana na Mchungaji Mwasapile ili kuweka utaratibu mzuri wa kutoa tiba hiyo kulingana na idadi ya watu.Wakati huohuo; Jeshi la Polisi mkoani Arusha kwa kushirikiana na wasafirishaji wa abiria kwenda Samunge, wameanza kuweka utaratibu wa kusimamia magari yanayokodiwa.



Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye alisema jana kuwa utaratibu unaandaliwa wa kuratibu magari yote yanayokwenda Loliondo kutoka Arusha katika kituo maalumu. Hiyo imetokana na kuwapo kwa taarifa kwamba kuna magari yanayowatapeli abiria na kuwatelekeza njiani baada ya kuchukua fedha.



Mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni ya Usafirishaji ya Shufaa ambayo hupeleka watu Loliondo, Saidi Kakiva alisema wamekubaliana kusajili magari yote ambayo yanakwenda Loliondo.



“Kumeibuka tabia ya kutelekeza wagonjwa na wengine kutupwa porini, hasa wale wanaofariki, hivyo sasa magari yanaandikwa namba na madereva wanaandikwa majina ili kuwadhibiti,” alisema Kakiva.



Kuhusu ombi la kumtaka Mchungaji Mwasapile ahamishie huduma zake Arusha, baadhi ya ndugu na jamaa za wagonjwa waliokwama katika barabara iendayo Samunge, wamesema hilo linaweza kuwa katika kipindi hiki ambacho barabara ya kwenda nyumbani kwake imeharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha.



Mmoja wa wananchi hao, Josephat Mwangoka anayetokea Dar es Salaam akimpeleka baba yake mzazi alisema: “Tunamuomba sana Mchungaji ahamishie shughuli zake walau Arusha mjini ili watu waweze kumfikia kwa urahisi hasa katika kipindi hiki ambacho mvua zimeharibu barabara. Hivi sasa watu wanatumia gharama kubwa mno kwenda kumuona kutokana na matatizo ya barabara.”


source:mwananchi communication

KAROTI; KINGA DHIDI YA SARATANI, UGONJWA WA MOYO

Na charles nazi

Kwa ujumla wake, karoti ni mboga yenye kiasi kingi cha Vitamini A. Mbali ya vitamini hiyo, karoti ina virutubisho vingine muhimu vyenye uwezo wa kuzuia magonjwa hatari, kama vile saratani, moyo na mengine mengi na kumbuka kwamba; ‘kinga ni bora kuliko tiba’.



Sifa pekee na kubwa kuhusu karoti inayojulikana na watu wengi, ni uwezo wake wa kuimarisha nuru ya macho na uwezo wa kuona, hususan wakati wa usiku. Katika makala ya leo nitakufahamisha faida nyingine za mboga hii rahisi, inayopatikana kwa wingi, mijini na vijijini. Ukiielewa vizuri, itaokoa maisha yako.









VIRUTUBISHO VYA KAROTI

Kwa mujibu wa tafiti kadhaa zilizofanywa, imethibitika kuwa karoti ina kiwango kikubwa cha virutubisho jamii ya ‘carotenoids’ ambavyo husaidia kuupa mwili uwezo wake wa asili wa kupambana na maradhi yanayojitokeza mwilini.



Katika utafiti huo, imeelezwa kuwa ulaji wa karoti, hata kwa kiasi cha karoti moja tu kwa siku, kinampunguzia mlaji uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa saratani ya matiti kwa asilimia 20.



Aidha, imeainishwa zaidi kuwa, mlaji wa karoti moja kwa siku, atakuwa pia anajiepusha na kupatwa na saratani za aina nyingine kwa asilimia 50. Saratani hizo zimetajwa kuwa ni saratani ya kibofu cha mkojo, kizazi, utumbo, mapafu na saratani ya koo.



Katika utafiti wa hivi karibuni wa Taasisi ya Saratani ya Taifa nchini Marekani (National Cancer Institute), imebainika kuwa wagonjwa wengi waliogundulika na saratani ya mapafu, katika milo yao walikuwa hawatumii karoti wala vyakula vingine vyenye virutubisho jamii ya ‘carotenoids’.



KAROTI NA UGONJWA WA KISUKARI

Kama tujuavyo, ugonjwa wa kisukari ni maradhi yanayowasumbua watu wengi duniani na hauna tiba. Magonjwa kama kisukari, huweza kumpata mtu kutokana na mpangilio mbaya wa vyakula anavyokula kila siku na staili ya maisha anayoishi kwa ujumla.



Mtu anaweza kujiepusha na magonjwa mengi hatari, kama kisukari, kwa kuzingatia ulaji usahihi. Kutokana na kiwango cha virutubisho mbalimbali vilivyomo kwenye karoti, mgonjwa wa kisukari anaweza kupata ahueni kwa kufanya karoti kuwa sehemu ya mlo wake wa kila siku.



Watafiti wamegundua kwamba virubisho vilivyomo kwenye karoti, vina uwezo mkubwa wa kurekebisha kiwango cha sukari mwilini, hivyo kutoa kinga au kumpa mgonjwa nafuu kubwa.



KAROTI NA MAPAFU

Kama unaishi au unafanya kazi katika mazingira yenye moshi au wewe ni mvutaji wa sigara, ulaji wa vyakula vyenye vitamin A kwa wingi kama karoti, humuepusha mvutaji na uwezekano wa kupatwa na saratani ya mapafu. Ulaji wa vyakula aina hii kwa mvuta sigara, si wa hiyari kama anataka kujiepusha na saratani ya mapafu.



JINSI YA KUCHAGUA NA KUHIFADHI KAROTI

Kwa kawaida, karoti huwa ni mzizi ulionyooka wenye rangi za kung’aa. Zipo karoti za rangi tofauti lakini karoti bora ni ile tuliyoizoea yenye rangi ya chungwa na kwa mujibu wa utafiti, karoti yenye rangi iliyoiva sana ndiyo yenye virubisho vingi zaidi.



Karoti inaweza kudumu kwa muda mrefu ikihifadhiwa vizuri. Hifadhi karoti yako kwenye jokofu ikiwa kwenye mfuko wa plastiki ambao hauruhusu kupitisha hewa nyingine, ikihifadhiwa vyema, karoti inaweza kukaa hadi wiki mbili bila kuharibika.



Aidha, wakati wa kuhifadhi karoti yako katika jokofu, usichanganye na matunda mengine kama vile ‘peasi’, nyanya, ‘epo’ na matunda mengine ya jamii hiyo. Inaelezwa kuwa kwa matunda hayo kukaa pamoja, kunaweza kuifanya karoti kuwa chungu.



Kabla ya kuhifadhi karoti kwenye jokofu, hakikisha umekata majani yake ya juu na mizizi yake ya chini, ili kuzuia karoti kuchipua licha ya kuwa kwenye jokofu.



JINSI YA KUANDAA NA KUILA KAROTI

Osha vizuri karoti yako kwa kutumia kifaa maalum cha kusugulia pamoja na maji safi. Wakati wa kuosha karoti, ni vizuri ukitumia maji ya kutiririka na siyo yaliyotuama. Osha karoti kwenye maji ya bomba au kwa kumimina na chombo, usioshee ndani ya chombo kuepuka kuondoka na vijidudu.

Itaendelea wiki ijayo.




Phenicia

Wednesday, March 16, 2011

Tusherehekee dawa ya Loliondo kwa hadhari kubwa

Tuesday, 15 March 2011 21:19

0diggs

digg

Mchungaji Ambilikile Mwasapile

KAMA kuna tukio ambalo liliwahi kugusa hisia na maisha ya wananchi wengi katika historia ya nchi yetu, basi tukio hilo ni kupatikana kwa dawa inayosemekana inatibu magonjwa sugu na yaliyoshindikana, yakiwamo Kisukari, Kansa na Ukimwi. Hakika, tunashindwa kupata maneno stahiki ya kuelezea jinsi Watanzania walivyopokea habari za kupatikana kwa tiba hiyo iliyoelezwa kupatikana katika Kijiji cha Samunge, wilayani Loliondo, mkoani Arusha.



Ni tukio lililoitikisa na linaloendelea kuitikisa nchi yetu wakati maelfu kwa maelfu ya wananchi, wazee kwa vijana, wanaume kwa wanawake wa itikadi na imani zote wakielekea kijijini Samunge kumuona Mchungaji Ambilikile Mwasapile ili awapatie tiba ya magonjwa hayo sugu. Ndio maana tunasema kuwa hilo ni tukio kubwa na la kihistoria, na ukubwa wa tukio hilo hasa unatokana na ukweli kwamba ni tukio la kiimani.



Kwamba Mchungaji huyo alioteshwa katika ndoto mwaka 1991 kuwa kuna dawa itakayoshushwa kwake ili aitumie kutibu magonjwa ambayo yameshindikana kutibiwa na binadamu. Mashuhuda wengi wanasema walitibiwa na dawa ya mchungaji huyo tangu alipoanza kutoa huduma hiyo mwaka 2009. Baadhi wamejitokeza hivi karibuni na kusema kuwa wamepona maradhi hayo sugu.



Na kama hiyo haitoshi, watu waliopata dawa ya Mchungaji Mwasapile tangu habari za tiba yake zilipochapishwa na gazeti hili kwa mara ya kwanza wiki iliyopita, wamesema dawa hiyo imewatibu na sasa wanaona wako fiti. Baadhi ya madaktari wamethibitisha kuwa wateja wao ambao awali walikuwa wanasumbuliwa na magonjwa hayo wamethibitika kupona baada ya kutumia dawa hiyo inayojulikana kwa jina la Mugariga.



Hicho hasa ndicho kielelezo cha sababu ya maelfu kwa maelfu ya wananchi kumiminika Loliondo wakitokea kila pembe ya nchi yetu wakifuata dawa hiyo inayosemekana ni ya ajabu. Pia hicho ndicho kielelezo cha akili, mawazo, macho na masikio ya Watanzania wote kuelekezwa katika Kijiji cha Samunge na kutekwa na nguvu anayosemekana kuwa nayo Mchungaji Mwasapile.



Na hasa hiyo ndio sababu ya Serikali kujikuta njia panda pasipo kujua la kufanya. Katika kuonyesha hali ya kuchanganyikiwa, Serikali kwanza ilitangaza kupiga marufuku shughuli za Mchungaji Mwasapile na baada ya wananchi kupaza sauti wakitaka huduma hiyo iendelee, Serikali ilisalimu amri mara moja hasa baada ya kutambua kuwa sauti za wananchi zilikuwa za kiimani zaidi.



Ni kwa sababu hiyo tunaipongeza Serikali kwa kutambua kuwa badala ya kuweka vizuizi ili maelfu kwa maelfu ya watu wasifuate tiba hiyo kijijini Samunge, ilikuwa busara kuwawezesha watu wapate tiba hiyo. Serikali ilifanya vyema kugundua kuwa maelfu ya watu waliokuwa wanafuata tiba hiyo wasingeogopa vizuizi au vitisho vyake, kwani baadhi yao walikuwa wamekata tamaa kutokana na maradhi sugu yaliyokuwa yanawasumbua, hivyo walikuwa tayari kwa lolote, hata kufa.



Vilevile, Serikali iligundua kuwa isingekuwa na askari wa kutosha kusimamia amri zake kwa sababu askari wengi walikuwa njiani kuelekea kijijini Samunge na wengine tayari walikuwa wamewasili huko kupata dawa hiyo. Pia, baadhi ya mawaziri, wabunge na watendaji wakuu serikalini walikuwa miongoni mwa wananchi waliokuwa wanafuata dawa hiyo.Ndio sababu tangazo la Serikali kuruhusu shughuli hizo za tiba kuendelea ziliwapa watu wengi faraja na matumaini makubwa.



Sisi tunawahadhalisha wananchi na Serikali kuwa, pamoja na tiba hiyo kuwa suala la kiimani, tusifanye makosa kuanza kufanya sherehe. Tunawashauri wananchi wote kwanza waipe dawa hiyo muda wa kutosha ili itoe matokeo na baadaye wataalamu wa afya wayathibitishe pasipo shaka.



Kwa upande mwingine, tunawashauri wale wanaohisi wameponywa au hawajaponywa na dawa hiyo wajitokeze kutoa ushuhuda ili mamlaka husika ziweze kufanya tathmini na kuwapa wananchi maelekezo stahiki. Ni imani yetu kuwa watakaoponyeshwa na dawa hiyo hawatafanya vitendo hasi, bali watamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwaletea nuru mpya.







Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Serikali, Ndesamburo watimiza ahadi Loliondo

Monday, 14 March 2011 21:37

0diggs

digg

Wananchi mbalimbali wa mji wa Moshi na vitongoji vyake wakijiandikisha katika ofisi za Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini, Philemon Ndesamburo kwa ajili ya kwenda Loliondo kupata tiba ya dawa kwa mchungaji Ambilikile Mwasapile. Picha na Dionis Nyato

Waandishi Wetu

SERIKALI imeanza kutimiza ahadi yake ya kumsaidia Mchungaji Ambilikile Mwasapile (76) anayedaiwa kutoa tiba ya magonjwa sugu katika Kijiji cha Samunge, Loliondo, mkoani Arusha baada ya kutoa mashine ndogo ya kufua umeme (jenereta) na kupeleka wauguzi na askari wa kutosha.



Wiki iliyopita, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisema Serikali ilikuwa inaandaa utaratibu wa kutuma idadi ndogo ya wauguzi ambao wangesaidia kutoa huduma kwa watu watakaohitaji ambazo zingekuwa nje ya zile zinazotolewa na Mchungaji Mwasapile. Aliahidi kupeleka gari la kubebea wagonjwa (ambulance) kijijini humo ili kutoa msaada wa haraka kwa watu watakaohitaji huduma hiyo.



Kutokana na mchango huo, kazi ya ugawaji wa dawa hiyo kuanzia juzi ilikuwa ikienda kwa haraka zaidi tofauti na awali. Pia sasa wagonjwa mahututi wanafikishwa kwanza kwa wauguzi kabla ya kupelekwa kwa mchungaji huyo Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).Pia Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wameweka kambi jirani na nyumba za Mchungaji Mwasapile na wamekuwa wakisimamia magari na hata kusaidia kusambaza vikombe vya dawa kwenye magari hayo ili kuondoa msongamano.



Aidha, kupatikana kwa huduma hiyo ya umeme, hivi sasa Mchungaji Mwasapile ameanza kufanya kazi hadi usiku, kutokana na Serikali kupitia Halmashauri ya Ngorongoro, kumkabidhi jenereta hiyo. Sasa inasaidia kupatikana kwa mwanga wa kutosha katika eneo analotoa tiba na nyumbani kwake.



“Naishukuru sana Serikali kwa kuleta umeme hapa na kuna wauguzi wamekuwa wakisaidia watu wanaokuwa mahututi, ila bado kuna tatizo la vyombo vya kuchemshia na kutolea dawa kutokana na ongezeko kubwa la watu,” alisema Mchungaji Mwasapile.Mwenyekiti wa Kijiji cha Samunge, Michael Lengume alisema tayari Serikali ya Kijiji hicho kwa kushirikiana na viongozi wengine wameunda kamati mbalimbali za kukabiliana na wingi wa watu.



“Kijiji chetu kina kaya 500, sasa. Wingi wa watu ambao unafikia hadi 30,000 kwa siku ni janga na ndiyo sababu tumejipanga kuhakikisha hakuna madhara ambayo yanatokea,” alisema Lengume na kutaja moja ya kamati hiyo kuwa ni ya afya, usafi na mazingira.“Pia tumehamamisha watu kuleta vyakula hapa na huduma nyingine na sasa chakula kipo. Hakuna sababu mtu kutoka Dar es Salaam kuja na chakula chake,” alisema Lengume.



Alitoa wito kwa kampuni za simu kupeleka minara ya mawasiliano japo ya muda ili kuondoa adha ya watu kukosa mawasiliano na ndugu zao wakiwa kijijini hapo.Mwandishi wa habari hizi juzi aliwashuhudia wauguzi wakiwabeba wagonjwa kwenye machela na kuwapeleka kunywa dawa kwa mchungaji Mwasapile na baadaye kuwabeba na kuwarejesha katika Zahanati ya Samunge kupumzika.



Tatizo kubwa sasa ni jinsi ya kufika kwa mchungaji huyo na kuna wasiwasi kwamba kama mvua zikiendelea kunyesha itakuwa vigumu kwa wananchi kufika huko kupata huduma. Tatizo ni kubwa hasa kwa wananchi wanaotumia Barabara ya Kigongoni, Engaruka, pembezoni mwa Mlima Oldonyolengai, Digodigo hadi kufika Samunge.



Akizungumza kwa simu kutoka Arusha baada ya kutoka Semunge kupata matibabu, mwananchi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Stella Ludovick alisema pamoja na misaada mingine ya kibinadamu, ujenzi wa barabara ya kuelekea katika kijiji hicho ni muhimu zaidi."Ndiyo, misaada hiyo mingine ni muhimu lakini, barabara ni tatizo la msingi kabisa. Serikali inapaswa kulishughulikia haraka tatizo la barabara kama kweli ina nia ya kusaidia huduma ya babu huyo," alisema Stella.



Alisema ilimchukua saa tisa kutoka Arusha hadi kijijini Semunge... "Barabara ni mbaya sana na kimsingi hili ndilo tatizo kubwa. Sisi tuliondoka Arusha saa 4:00 usiku na kufika kijijini huko saa 3:00 asubuhi ya siku iliyofuata. Saa tisa mtu uko njiani."Magari yanayotumika ni magari ya watalii ambayo mvua ikinyesha, hayawezi tena kwenda.



Nauli yake kutoka Arusha hadi Loliondo ni Sh150,000 kwa abiria. Zamani magari hayo yalikuwa yakisubiri abiria lakini kutokana na msongamano wa wagonjwa hili limekuwa haliwezekani tena. Mfanyabiashara gani atasubiri juma moja kupata tiba?"



Alisema maeneo mengi ya barabara hiyo ni mabaya kutokana na kujaa vumbi na mashimo, huku wingi wa magari yanayosafirisha wagonjwa kuelekea katika kijiji hicho yakiongeza tatizo hilo.



Ndesamburo atimiza ahadi

Mbunge wa Moshi Mjini, Phillemon Ndesamburo ametimiza ahadi ya kutoa usafiri bure kwa wakazi wa jimbo hilo kwenda Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile.Ndesamburo aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tangu kuanza kwa huduma hiyo amegundua kuwa wananchi ndiyo wanaopata shida zaidi kufika Loliondo.



Alisema baada ya kuguswa na tatizo hilo, ametoa magari mawili aina ya Bedford na Youmork yenye uwezo wa kubeba wagonjwa 73 ambayo yataanza kutoa huduma kesho. Hata hivyo, Ndesamburo alikuwa ameahidi kuwapeleka wananchi wa jimbo lake huko Loliondo kwa helikopta yake kabla ya kubadili uamuzi huo na kutumia magari hayo makubwa.



Alisema msaada huo hauhusiani na itikadi za chama cha siasa. Usafiri huo ni kwa ajili ya wakazi wa Moshi Mjini na vinatumika vitambulisho vya kupigia kura kuwabaini.Ndesamburo alifafanua kuwa wakazi hao watatakiwa kujitegemea chakula, maji na Sh500 ya kumlipa mchungaji huyo.



Mbunge huyo alisisitiza kuwa huduma hiyo si ya muda mfupi hivyo kuwatoa wasiwasi wakazi ambao wamekuwa wakigombea kwenda katika awamu ya kwanza kwa hofu kuwa inaweza iwe ndiyo mwisho.

Habari hii imeandikwa na Kizitto Noya, Dar; Mussa Juma, Loliondo na Fina Lyimo, Moshi.

Rostam aponda tiba ya Mchungaji Loliondo

Tuesday, 15 March 2011 21:22

0diggs

digg

Shija Felician, Igunga

WAKATI Watanzania wengi wakimiminika kwenda wilayani Loliondo, mkoani Arusha kupata dawa inayodaiwa kutibu magonjwa sugu, Mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz ameibuka na kusema tiba hiyo haina lolote akidai kwamba ndugu zake watano wameitumia lakini hawajapona.



Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wapigakura uliofanyika kwenye Viwanja vya CCM wilayani Igunga, Tabora mbunge huyo alisema haiamini dawa hiyo kwa kuwa ana ushahidi kwa ndugu zake hao ambao anadai kwamba wanaendelea kuugua kisukari licha ya kutumia dawa hiyo siku saba zilizopita.



Aliwataka wale watakaokwenda Loliondo ambao wanatumia dawa za hospitalini kuendelea kuzitumia badala ya kuzipuuza na kuzitupa... “Ndugu zangu wananchi wa Igunga, mimi mjomba wangu Hassan mnamfahamu karibu wote hapa mjini ni mgonjwa wa siku nyingi wa kisukari. Ameshakunywa dawa hiyo lakini mpaka sasa ni mgonjwa kama mnavyomuona sasa hiyo dawa inaponyesha nani?”



Hata hivyo, aliwataka wananchi wote wenye imani juu ya dawa hiyo waende huku akiwasisitizia kutopuuza ushauri wa madaktari kwani.



Wakati Rostam akipinga dawa hiyo, wilayani Kahama, mamia ya wafanyabiashara wamefunga shughuli zao na kukimbilia Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile kunywa dawa hiyo huku baadhi ya waliorejea baada ya kuinywa wakidai kuwa hali zao sasa ni nzuri.



Wafanyabiashara hao wengi wao wanaondoka kwa siri wakidai wanakwenda Dar es Salaam katika shughuli zao, lakini siri imefichuka baada ya baadhi yao kuoneka katika runinga wakiwa katika foleni wakisubiri kupatiwa huduma hiyo.



Mbali ya kuzungumzia suala hilo la tiba ambalo limegusa hisia za wananchi wengi wa Afrika Mashariki, mbunge huyo aliwapa pole wananchi wa Igunga ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha wiki iliyopita ambazo ziliathiri kaya 19. Aitoa msaada wa Sh500,000 kwa kila kaya iliyokumbwa na maafa hayo.





Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Lowassa apata kikombe Loliondo kwa babu

Tuesday, 15 March 2011 23:47

0diggs

digg

Waandishi Wetu

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.



Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.



Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.



Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”



Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.



Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.Lowassa ni miongoni mwa wanasiasa maarufu nchini ambao wameshafika kwa mchungaji huyo kupata tiba hiyo wakiwamo mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya.





Katika jitihada za kudhibiti usalama na kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma kwa mchungaji huyo bila matatizo, Serikali imeimarisha ulinzi kwa kuweka askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), katika kijiji hicho na kusimamia magari. Pia imepeleka wauguzi kusaidia wagonjwa mahututi kabla ya kumfikia mchungaji na imetoa pia jenereta kwa ajili ya kufua umemeKaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Raymond Mushi alisema jana kuwa, sasa walau hali ni nzuri kwani msongamano umepungua.





"Ni kweli sasa hali inaridhisha na jana watu wamekwenda kupata tiba na kurejea makwao mapema hili ndilo serikali inalolitaka. Tunaomba watu wanaopeleka wagonjwa wawe wanauliza kwanza hali ya msongamano," alisema Mushi.Mushi alisema inawezekana watu wanaokwenda katika kijiji hicho kusubiriana katika Mji wa Mto wa Mbu ambako kuna huduma nyingi muhimu kuliko wote kwenda huko kwa wakati mmoja.



Alitoa wito kwa watu wenye wagonjwa mahututi kuacha kuwapeleka moja kwa moja kwa mchungaji huyo kabla ya kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu afya zao.Katika hatua nyingine, wagonjwa kadhaa waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wameanza kutoroka wodini na kwenda Loliondo kupata matibabu ya magonjwa sugu yanayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapile, Mwananchi imeelezwa.



Habari zilizopatikana hospitalini hapo jana zimeeleza kuwa wagonjwa hao walianza kuondoka Muhimbili juma lililopita baada ya Serikali kubariki matibabu hayo. Ofisa mmoja mwandamizi wa hospitali hiyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini, amesema kuwa wakati baadhi ya wagonjwa hao wakiwa wanatoroka wodini, wengine wamekuwa jasiri kwa kuwaaga madaktari wao.



“Wagonjwa wameanza kuondoka na wengine bila hata ya kuaga, hivyo hatujui hatima yao kama watafika salama huko Loliondo,” alisema.Ofisa huyo alisema juma lililopita, mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa chumba namba 15 katika Wodi ya Kibasila, aliondoka baada ya kusikia taarifa kuhusu huduma hiyo.



“Kuna mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa Kibasila Wodi namba 15 aliondoka aliposikia kuwa Babu ameanza tena kutoa matibabu hayo ambayo awali yalisitishwa,” alisema.Hata hivyo, Ofisa Habari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaisha alisema hana taarifa za kutoroka wodini kwa wagonjwa hao na kwenda kufuata tiba huko Loliondo... “Sina taarifa zozote za kuondoka kwa wagonjwa hapa hospitalini.”



Matibabu Loliondo yapandisha nauli Ubungo

NAULI za kwenda Arusha kutoka Ubungo, Dar es Salaam zimepanda kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na wingi wa wasafiri wanaoelekea Loliondo kupata tiba hiyo ya magonjwa sugu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana kutoka kituoni hapo zimeeleza kuwa, nauli hizo zimepanda kutoka Sh18,000 hadi Sh30,000 tangu juma lililopita.



Mmoja wa mawakala wa mabasi ya abiria katika kituo hicho ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema ongezeko hilo la nauli limetokana na baadhi ya mawakala kukodi mabasi na kuwasafirisha abiria.“Nikupe siri moja tu ambayo inatufanya tupandishe nauli. Lengo letu ni kupata faida, ujue sisi tunakodi basi zima kisha tunakatisha tiketi kwa bei yetu ili na sisi tupate faida,” alisema.



Mmoja wa abiria aliyekuwa akisafiri kuelekea Arusha, Charles Manyama alisema mabasi yaendayo huko yamegawanyika katika madaraja matatu yale ya bei ya juu, bei ya kati na bei ya chini lakini kwa sasa bei imekuwa ni moja kwa mabasi yote.



Kwa mujibu wa abiria huyo, zamani nauli za Arusha zilikuwa Sh25,000 kwa basi la daraja la juu, Sh18,000 kwa mabasi ya daraja la kati na Sh15,000 kwa daraja la chini, lakini sasa mabasi yote yanatoza kati ya Sh25,000 hadi Sh30,000.“Mawakala hawa wanadhani kila mtu anayepanda magari haya anakwenda Loliondo lakini siyo kweli, wengine tuna safari nyingine kabisa," alisema Manyama na kuongeza:



"Unakuta bei zinashangaza na kupanda sana. Hata hivyo, inashangaza kuona wanadamu tunakosa utu. Watu wanakwenda kupata matibabu wanapandishiwa nauli, walipaswa kuwaonea huruma wagonjwa hawa,” alisema Manyama.Jitihada za kumtafuta Meneja wa kituo cha mabasi Ubungo ziligonga mwamba baada ya taarifa kutoka ofisi kwake kueleza kuwa alikuwa nje kikazi.



Polisi Arusha wadhibiti usafiri wa Loliondo

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limeitaka Halmashauri ya Jiji la Arusha kuweka vituo vinavyotambulika kwa ajili ya wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu kwa Mchungaji Mwasapile ili kuepuka utapeli.



Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alisema jana kuwa kutokana na idadi kubwa ya watu kutaka kwenda Loliondo, kumezuka vituo vingi ambavyo vinaweza kuwa chanzo cha utapeli kwa watu wanaotoka mikoani."Nafahamu hili ni jambo ambalo manispaa wanahusika nalo, wahakikishe kuwa hakuna vituo visivyo rasmi ili wananchi wasije kudanganywa na watu wabaya," alisema.



Katika kituo kilichoibuka ghafla baada tiba ya magonjwa sugu kuanza kutolewa cha Chini ya Mti, kulizuka vurugu za madereva na madalali waliokuwa wakibishania kiwango cha nauli, hatua iliyosababisha polisi wenye silaha kupelekwa katika eneo hilo.



Hatua ya polisi kuonekana katika kituo hicho, ilisababisha wasiwasi kwa wananchi kuwa huenda Serikali imesimamisha utaratibu wa wananchi kwenda Loliondo, jambo ambalo kaimu kamanda huyo alilikanusha.



"Tunachokifanya ni kuweka utaratibu mzuri, polisi wanasimamia sheria. Magari mengine yanazidisha idadi ya watu na kutoza pesa nyingi zaidi. Sumatra wakisema nauli sahihi ni kiwango fulani na madereva wakizidisha basi tunawakamata," alisema.



Wananchi waliozungumza na gazeti hili bila kutaja majina yao walisema kuwa wanashangazwa na bei ya nauli kuwa juu hata baada ya Serikali na KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Kati kuboresha mazingira ya kuwahi kupata tiba na kuondoka kijijini Samunge.



"Mwanzoni walikuwa wanasema magari yanakaa sana huko, kwa hiyo wanafidia hizo siku za kungoja wagonjwa lakini sasa hivi ukienda leo unarudi kesho na nauli bado iko juu," alisema mmoja wa wananchi hao.Nauli ya kutoka Mjini Arusha hadi Samunge, Loliondo ni Sh100,000 kwenda na kurudi kwa magari aina ya Land Cruser ,huku nauli ya mabasi ikiwa pungufu zaidi.



Habari hii imeandaliwa na Nevile Meena, Ibrahim Yamola, Dotto Kahindi Dar na Mussa Juma, Filbert Rweyemamu, Arusha

Tuesday, March 15, 2011

ACHA BABU AITWE BABU-NA ASHUKURIWE MUNGU

Mussa Juma, Loliondo na Deusdedit Moshi, Dodoma






DAKTARI Joachiam Mbosha wa Hospitali Teule ya Wilaya ya Ngorongoro ya Wasso, amethibitisha kuwa mmoja wa wagonjwa wa Ukimwi aliyekwenda kutibiwa kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapile, maarufu kwa jina la 'Babu', huko Samunge, Loliondo amepona Ukimwi.

Wilia John Lengume (30), juzi alikuwa kivutio kwa mamia ya watu baada ya kutangazwa na Mchungaji Mwasapile kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Usharika wa Sonjo iliyoshirikisha mamia ya watu. Akizungumza katika ibada hiyo, Mchungaji Mwasapile alisema Lengume ndiye aliyekuwa mgonjwa wa kwanza kumtibu.



Akizungumza na Mwananchi kanisani hapo, Lengume alisema baada ya mumewe, John Meneyi Lengume kufariki dunia mwaka 2002, aliamua kwenda kupima na kuonekana kuwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) lakini baada ya kutumia dawa hiyo alisema sasa hana tena virusi vya Ukimwi. Alisema kwa muda mrefu mama huyo alikuwa akitumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo (ARV) katika Kituo cha Afya Didodigo wilayani Ngorongoro.



Akizungumza na Mwananchi jana kuhusu kupona kwa mama huyo, Dk Mbosha alisema: “Hiki kitu kilituchanganya sana, nakumbuka mimi ndiye nilimpima mwaka jana... ikabidi niwaeleze watu wa maabara Hospitali ya Wasso ili wafuatilie aliyempima awali huyu mama na nilimweleza aache kutumia dawa kwani hana HIV,” alisema Dk Mbosha.



Dk Mbosha alisema alihamishiwa katika kituo hicho cha Afya cha Digodigo zaidi ya mwaka mmoja uliopita na alimkuta mama huyo akiendelea kuhudhuria kliniki na kupata ARV pamoja na ushauri wa kulinda afya yake lakini alianza kuona mabadiliko makubwa ya afya yake na ndipo alipoamua kumpima tena.



Aliamua kumpima mwaka jana baada ya kuona 'CD4' (kinga za mwili) zake zinaimarika kiasi cha kutohitaji kuendelea kutumia dawa hizo za kupunguza makali.Aliamua kumhoji kujua siri iliyokuwa imejificha katika mabadiliko hayo ambayo alisema yalikuwa ya haraka haraka mno na ndipo alipomweleza kwamba alipata tiba kutoka kwa Mchungaji Mwasapile.



Lengume alisema licha ya mumewe kufariki, mtoto wao mmoja pia alifariki dunia lakini baada ya kutumia dawa ya Mchungaji Mwasapile, maisha yake ni mazuri na ana mtoto mwingine mchanga anayeitwa Evelyn ... “Namshukuru Mungu na Mchungaji Mwasapile sasa nimepona na ninaishi maisha mazuri tu.”Alisema baada ya kuanza kuugua, mchungaji huyo, ndiye aliyemfuata na kumuomba amtibu akimthibitishia kwamba atapona maradhi yaliyokuwa yakimsibu.Hata hivyo, kitalaamu bado haijathibitika kupatikana kwa tiba wala chanjo ya Ukimwi.



Ushuhuda wa Mzee Mtaki

Mwingine aliyejitangaza kupata ahueni kubwa kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimsibu baada ya kupata tiba ya mchungaji huyo ni aliyewahi kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, Mzee Ali Said Mtaki.Mzee Mtaki (81) ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Mpwapwa katika miaka ya 1980, Mkuu wa Mikoa ya Dodoma na Singida kwa nyakati tofauti, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mbunge wa Afrika Mashariki na kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Usharika Mkoa wa Dodoma, alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya kutetemeka kiasi cha kushindwa kutembea na kuzungumza vizuri.



Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake Mtaa wa Nyerere Mjini Dodoma, Mzee Mtaki alisema tangu anywe dawa ya mchungaji huyo Jumanne ya wiki iliyopita huko Loliondo, sasa anaendelea kupata nafuu siku hadi siku.



Akiongea kwa kujiamini alisema sasa anajiona kama amepona na anaweza kuendelea na shughuli zake ikiwamo ya uwakala wa bima... "Si unaona nilikuwa natembea kwa shida, kuzungumza kwa taabu, sasa hali yangu ni nzuri nafanya kila kitu bila kusaidiwa.”Akielezea safari yake ya siku mbili ambayo ilimfikisha kijijini Samunge, Loliondo anasema alifuatana na mkewe, Amina Mtaki ambaye naye alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na mgongo. Anasema naye pia amepona.



Anasema safari ya kutoka Dodoma hadi Samunge iliwagharimu Sh60,000 kila mmoja na baada ya kufika huko walikuta umati mkubwa wa watu ukisubiri kupata tiba hiyo. Anasema aliwakuta watu wa mataifa mbalimbali, Waafrika, Wahindi, Wazungu na Waarabu... "Watu walikuwa wengi na kila mtu na matatizo yake lakini Mchungaji alikuwa akiwasisitizia kwamba habagui watu na haangalii dini au uwezo wa mtu."



“Katika mkusanyiko huo nilibahatika kukutana na Askofu Thomas Laizer wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Kati akiwa amefuatana na mama wa kizungu. Nilikaa karibu na mama yule wa kizungu ambaye sikumbuki jina lake. Nilimshika Askofu Laizer mkono tukasalimiana na kuongozana naye kuelekea kwa Mchungaji Ambilikile."



"Tulipofika kwa Mchungaji, Askofu Laizer akamwambia mchungaji kwamba ana wageni wake, hivyo mama yule wa kizungu akapewa dawa na mimi pia nikapewa na mke wangu akapewa pamoja na kijana wangu japo yeye hakuwa na tatizo lolote la kiafya."

Tuesday, March 8, 2011

Women Empowerment 2

Editor's note: Belinda Otas is a freelance journalist, writer and blogger with a special focus on Africa. She contributes to The New African and New African Woman magazines, where she writes extensively on women's issues, most recently the use of rape as a weapon of war in the Democratic Republic of Congo.




(CNN) -- Today is the 100th anniversary of International Women's Day, a milestone centenary worthy of the celebrations bestowed upon it. Michelle Bachelet, the first executive director of U.N. Women and former Chilean president, has described the last century as one of progress and of "women using their collective voice to organize for change."



There is nothing wrong with celebrating women's achievements and contributions to society. A lot has happened since 1911, from the recognition of women's right to vote to more political participation and the election of female leaders like Liberian President Ellen Johnson-Sirleaf, and most recently, Dilma Rousseff of Brazil.



Women are mobilizing alongside their male counterparts for greater political freedom like we have seen in Egypt and Tunisia. Women are robustly active in the workforce and serve as CEOs of Fortune 500 companies.



However, on the African continent, urgent work is needed to address the ills of gender inequality, marginalization and social injustice currently endured by women in places like the eastern Democratic Republic of Congo, where violence against women is rife and rape has become a weapon of war. In addition, a rise in child trafficking has led to an increase in prostitution, domestic abuse, the continued practice of female genital mutilation and forced and early marriage of girls.



After 100 years and landmark resolutions, surely we should be closer to achieving the results of these various mandates.



--Belinda Otas

RELATED TOPICS

Women's Issues

African Politics

Democratic Republic of the Congo

Liberian Politics

Rwanda

United Nations

At the end of the civil war in Liberia, it is estimated that as many as 60% to 90% of the nation's women and girls had been raped. In Rwanda, an estimated 100,000 to 250,000 women suffered the same fate during the genocide of 1994. On that occasion, the world made the promise of "never again" -- the very same words used at the end of the Jewish Holocaust of World War II.



But as the days go by, the harder it is to uphold that promise, best demonstrated in the DRC, which a top U.N. official called the "rape capital of the world" last year.



In 1975, the first U.N. World Conference on Women was held in Mexico City, where three core objectives were identified: Full gender equality and the elimination of gender discrimination; the integration and full participation of women in development; and an increased contribution by women towards strengthening world peace.



Since then, a slew of resolutions aimed at empowering women have been adopted. In 2000, the U.N. Security Council passed Resolution 1325, which calls for better protection of women and girls in conflict zones, and in 2008, it adopted Resolution 1820, which for the first time recognized rape as a weapon of war. In July 2010, U.N. Women, an organization that Bachelet calls "an ambitious international commitment to accelerate the realization of women's rights and gender equality," was created.



While these protocols exist, it cannot be claimed that Africa is closer to gender equality in the same proportion as its western counterparts. After 100 years and landmark resolutions, surely we should be closer to achieving the results of these various mandates.



In a recent interview with Zainab Salbi, founder of Women for Women International, a nonprofit that helps women in war-torn regions, I asked her if the U.N. had become complacent where the use of rape and violence against women is concerned.



She said there was a high level of tolerance because while the U.N. has laws, resolutions and guidelines about women's issues, it doesn't really "get the whole issue about the provision of security for women and children. There needs to be a complete protection plan. It's doable if there is political will."



That political will is absent at national levels on the African continent. No one denies that some progress is being made. The sentencing of Lt. Col. Kibibi Mutware to 20 years in jail last month for the mass rape of women in the village of Fizi in the DRC is an overdue step in the right direction.



However, it is time African governments and the U.N. take radical action that ensures that resolutions gathering dust on the shelves are translated into action -- a process that would involve educating and investing in women and serving them through the creation and expansion of social, legal and health structures and services.



There must be economic empowerment by means of viable opportunities that give women financial freedom and ensure perpetrators of rape and violence against women are brought to justice.



More important, African women must be brought in from the cold and empowered to become active political participants from the grassroots to national government levels, where key peace negotiations and decisions that affect them are made.



This is an area where Rwanda currently leads the rest of the world, with its 56.3% of female parliamentarians. Until this happens, President Johnson-Sirleaf writes in the winter edition of the New African Woman magazine, "the job of full equality and total empowerment is incomplete."



The opinions expressed in this commentary are solely those of Belinda Otas.

Income Inequality between Men and women

(CNN) -- The earnings gap between men and women has narrowed, but a new White House report shows that on average women still only make about 75% as much as their male counterparts.




The report released Tuesday shows that women have not only caught up with men in college attendance but in fact have surpassed them, yet that gain hasn't translated into the pocketbook. Statistics also show women are more likely than men to live in poverty.



This is the first comprehensive look at women's status in American society in more than 50 years, according to the Obama administration. Valerie Jarrett, White House counselor and chair of the White House Council on Women and Girls, calls the report "a guidepost to help us move forward," and also says the data will affect future policy decisions.



"I think it will inform a wide variety of different policy in programs that the federal government will either initiate or continue but it will be evidence-based," Jarrett said during a conference call Tuesday with reporters. "(We'll) look at those programs and how they fit together to improve the quality of lives of women as a whole rather than looking at it in a silo," she said.



Women's incomes now account for about one-third of their family's total take-home pay. Jarrett said that fact highlights that this is not simply a women's study but rather one showing how a woman's life affects society as a whole.



"(We) realize we have got to encourage women to go into higher paying fields or be educated in a way that's going to lead to higher paying jobs," she said. "You really have to look at the whole story of a woman's life and I think this report gives us comprehensive framework to do that. "



As women contribute more to the family budget, some are out-earning their husbands. The study shows 18% of working women earned more than their spouses. There have also been changes in family life. Fewer women are married. In 2009, 62% of women were married. That's down from 72% in 1970. In addition, in 2009, 15% of women had never been married.



The report also shows that today's woman is having fewer children than in the past and she is having her first baby at an older age. Today 22% of women are having their first child in their 30s compared to only 4% of women in the 1970s. More women in their 40s are first-time mothers than ever before.



The report also says that fewer women are targets of violent crime, including murder. But still women are more likely to be victims of some crimes including stalking and domestic violence.



The report analyzes women's role in families and income, education, employment, and crime and violence.



The Office of Management and Budget and Department of Commerce drew together data from more than a dozen agencies across the federal government to put together the report. The study was launched to support he White House Council on Women and Girls that was created by President Barack Obama two years ago.



The White House is releasing the report in connection with March being Women's History month.

Women Day Celebration Day Does equality there yet?????????

Editor's note: Stephanie Coontz teaches history at the Evergreen State College in Olympia, Washington, and most recently authored "A Strange Stirring: The Feminine Mystique and American Women at the Dawn of the 1960s ."




(CNN) -- Last week the White House released a comprehensive statistical report on "Women in America: Indicators of Social and Economic Well-Being," the first such assessment since President John F. Kennedy's Commission on the Status of Women released its findings in 1963.



The new report indicates that women still earn less, on average, than men and are more likely to live in poverty. They are also at much greater risk of sexual assault and of violence at the hands of an intimate partner than men.



To be sure, the report shows that there is still plenty of progress to be made. But it is Women's History Month, and a good time to pause for perspective.



There have been astonishing improvements in the status of American women in the 48 years since the first report was published. For one thing, the authors of this year's report saw no need for a section detailing the legal disabilities facing American women.



By contrast, the 1963 report cataloged the array of laws and practices that denied homemakers any legal claim on money earned by their husbands and gave husbands the right to determine where a couple lived, how community property was spent, and even whether a wife could get a credit card.



Nor did this year's report need to complain about the once-common practice of establishing quotas on how many women were admitted to educational institutions or desirable jobs. In 1963, just 2.6 percent of all attorneys were female, and of the 422 federal judges only three were women. Today, women make up one-third of all lawyers, and there are three females on the U.S. Supreme Court.



In 1960, 60 percent of women who entered college quit before graduation, often to earn their Ph.T., as the practice of dropping out to Put Hubby Through school was jocularly called. Today at all educational levels, females are less likely than males to drop out of school. Women now earn a majority of bachelor's degrees, master's degrees and doctorates.



And unlike 1963, educational achievement now outweighs gender in determining income. As late as 1970, the average woman with a bachelor's degree, working full time, earned less than the average male high-school graduate. Today, in most major metro areas, women in their 20s earn more their male counterparts, largely because of their higher educational attainments.



Over the course of a lifetime, women generally still earn less than men, in large part because they are more likely than men to adjust their work schedules to the demands of raising children. For that, they pay an economic price that accumulates and accelerates over the years.



Women are also more likely to have residential custody of children after a divorce or unwed birth, which puts an added damper on their earning power. But it is worth noting that the poverty rates of divorced and unwed mothers were twice as high in 1963 as they are today.



There has been similar progress in terms of violence against women. Domestic violence rates fell by 54 percent between 1994 and 2008, and the rate of rape against women, as measured by self-reports and not just police reports, fell by 60 percent between 1993 and 2000.



I'm not arguing that we now live in a paradise for women. Gender barriers and stereotypes still get in the way of women's progress. In traditionally male fields such as engineering and computer sciences, females still receive only 20 percent of the degrees. Women still tend to be concentrated on lower-paid, traditionally "female" fields, such as teaching and nursing. Only a handful of CEOs of Fortune 500 companies are female.



Even when they do enter higher-paid occupations, many studies show that women are much less assertive than men about negotiating their salaries. Economists estimate this unwillingness to assert their own worth as workers ends up costing women as much as $500,000 in earnings by the time they reach 60.



This pattern, along with the continued existence of "old boy" networks, helps explain why more than three-quarters of all workers earning more than $100,000 per year are men.



But today adhering to gender stereotypes in the workplace can be costly for men as well as women. Many men, for example, still tend to shun "female" jobs in favor of work in the construction and industrial fields that are increasingly precarious in our society. As a result, in the past four recessions men have had higher unemployment rates than women -- a sharp break from past experience -- and are less likely to have health insurance than women.



Clearly, gender stereotypes still lead to behaviors that do harm. But increasingly they are harmful to men as well as women. One of the great achievements of the past five decades is that we have reached a point where the inequalities in our society are not something that all women and minorities face and only women and minorities suffer from.



But that is also our great challenge -- figuring out how to eliminate the inequalities that still remain.

Thursday, March 3, 2011

The Refugee Studies Centre’s International Summer School

The Refugee Studies Centre’s International Summer School fosters dialogue between academics, practitioners and policymakers working to improve the situation of refugees and other forced migrants. It provides the time and space for them to reflect on their experiences and to think critically about some of the aims and assumptions underlying their work.




The brochure of the Summer School is available in PDF format.



Who is the summer school for?



Policy makers and practitioners involved with humanitarian assistance and policy making for forced migrants. Participants typically include host government officials, intergovernmental and non-governmental agency personnel engaged in planning, administering and co-ordinating assistance.



Researchers specialising in the study of forced migration.



Why participate?

The summer school offers an intensive, interdisciplinary and participative approach to the study of forced migration. It aims to enable people working with refugees and other forced migrants to reflect critically on the forces and institutions that dominate the world of the displaced.



Now in its 22nd year, the three-week course combines the very best of Oxford University’s academic excellence with a stimulating and participatory method of critical learning.





The details



When?

Annually. In 2011 the dates are 11–29 July.



Where?

At the University of Oxford. In 2011 the summer school will be held at Wadham College and the Oxford Department of International Development.



How much?

The fee for 2011 is £3,125. Pay by 31 March to qualify for a reduced fee of £2,950.

What is included?

This covers 19 nights’ bed-and-breakfast accommodation and all weekday lunches; all tuition; all course materials, including reading materials; and a range of social activities.Evening and weekend meals are not included in the course fees.



Requirements

Applicants should have:



experience in working with, or on issues related to, refugees or other forced migrants

a first degree

proficiency in the English language. As a guide, foreign-language English speakers should be able to obtain a score of 7.00 in ELTS/IELTS or 570 in TOEFL.

Accommodation

Accommodation is of general student standard. There are no facilities provided for partners or other family members. Participants arriving before or staying on after the summer school should make their own accommodation arrangements.



Subsistence

As well as fees and travel costs, participants should budget for subsistence and incidental expenses during the course. We suggest a minimum of £20-£25 per day. In addition, you might want to add a books/photocopying allowance.



Sponsorship

A number of bursaries are offered on a competitive basis. Conditions for their allocation are dependent on the bursary providers' criteria, and are usually linked to certain poorer countries or regions. Some past participants have been successful in obtaining sponsorship by dealing directly with funding sources that they have researched themselves. We strongly advise potential applicants to look for funding as widely as possible, as we always receive many more bursary applications than we are able to offer.



Use of the RSC’s library collection

The programme provides a course pack of reading materials. Many more documents are available in the University of Oxford’s Social Science Library, which houses the RSC collection.



Insurance

Participants are responsible for their own insurance. Participants from outside the European Union should consider medical insurance if their country does not have a reciprocal agreement with the UK for free medical treatment.



How to apply

You can apply online, or by fax/post. Please use the application form (available online or as a Word document). All applications are reviewed by a selection committee. The closing date for applications is 1 March 2011 for applicants requesting a bursary through the RSC, 1 May 2011 for all other applicants. As the summer school is typically oversubscribed, we advise you to apply in good time.



Please send all applications and enquiries to



The International Summer School Manager

Refugee Studies Centre

Oxford Department of International Development

University of Oxford

3 Mansfield Road

Oxford, OX1 3TB, UK

tel: +44 (0)1865 281728

fax: +44 (0)1865 281730

email: summer.school@qeh.ox.ac.uk





IMPORTANT: For more information and the source, CLICK HERE

Hewlett Foundation/IIE Dissertation Fellowship in

Hewlett Foundation/IIE Dissertation Fellowship in


Population, Reproductive Health, and Economic Development













Before reading, please WATCH this video about this Fellowship





http://www.youtube.com/watch?v=bGHsgCKS620



The Institute of International Education (IIE) is now accepting applications for the Dissertation Fellowship in Population, Reproductive Health, and Economic Development. Sponsored by The William and Flora Hewlett Foundation, the fellowship awards up to $20,000 per year for work and research on the dissertation. In addition, Fellows will become part of a network of researchers and participate in professional development opportunities. Applicants should be currently enrolled in Ph.D. programs in either sub-Saharan Africa, the United States or Canada, and should have completed their coursework by the start of the fellowship. Students in economics, economic demography, geography, and epidemiology are especially encouraged to apply.







These fellowships will support dissertation research on topics that examine how population dynamics and family planning and reproductive health influence economic development, including economic growth, poverty reduction, and equity. Dissertations that address population and development issues pertinent to the African continent are especially encouraged. The research must include a strong quantitative component, with an emphasis on rigorous data analysis. We encourage the development or use of new statistical methods. Finally, the research must have a strong policy-relevant component, demonstrating an interest in communicating research results with program managers, planners, and policymakers.



The objective of The William and Flora Hewlett Foundation/IIE Dissertation Fellowship is to produce sound evidence on the role of population and reproductive health in economic development that could be incorporated into national and international economic planning and decision making.





To learn more about the fellowship, access the Application, and check for Fellowship related news, please visit our website at:

http://www.iie.org/en/Programs/Hewlett-IIE-Fellowship





The deadline is March 4, 2011. The selected cohort will be announced in late spring 2011.







Research that is not about the relevant subject matter will not be considered.



SOURCE: CLICKE HERE





MAKULILO, Jr.

California, USA

A new round of Newton International Fellowships

A new round of Newton International Fellowships – an initiative to fund research collaborations and improve links between UK and overseas researchers – has now opened.




The Newton International Fellowships are funded by the British Academy and the Royal Society and aim to attract the most promising early-career post-doctoral researchers from overseas in the fields of the humanities, the natural, physical and social sciences. The Fellowships enable researchers to work for two years at a UK research institution with the aim of fostering long-term international collaborations.



Newton Fellows will receive an allowance of £24,000 to cover subsistence and up to £8,000 to cover research expenses in each year of the Fellowship. A one-off relocation allowance of up to £2,000 is also available.





In addition, Newton Fellows may be eligible for follow-up funding of up to £6,000 per annum for up to 10 years following completion of the Fellowship to support activities which will help build long term links with the UK.



The scheme is open to post-doctoral (and equivalent) early-career researchers working outside the UK who do not hold UK citizenship.



Applications are to be made via the Royal Society’s online application system which is available at https://e-gap.royalsociety.org/



The closing date for applications is Monday 4 April 2011.



Further details are available from the Newton International Fellowships website: www.newtonfellowships.org or call 00 44 (0)20 7451 2559



Newton International Fellowships

6-9 Carlton House Terrace

London SW1Y 5AG

tel: +44 (0)20 7451 2559

fax: +44 (0)20 7451 2543

The British Academy, 10-11 Carlton House Terrace, London SW1Y 5AH Tel: 020 7969 5200, Fax: 020 7969 5300, Web: www.britac.ac.uk





SOURCE & Application: http://www.newtonfellowships.org/the-fellowships.aspx



MAKULILO, Jr.

California, USA

Four doctoral student positions

Uppsala University hereby invites applications for the following position:






Four doctoral student positions



At the Department of Law from 1 September 2011.



An employed doctoral student shall, foremost, be devoted to his or her own postgraduate research. Other duties at the faculty which relate to teaching and administrative work may be included within the scope of the employment (to a maximum of 20%).



A requirement for employment as doctoral student is that the applicant must be admitted to postgraduate studies. To this extent, the applicant’s ability to successfully complete the doctoral studies will be decisive. The regulations governing the employment of doctoral students may be found in Chapter 5, §§ 1-7 of the Higher Education Ordinance.





Local guidelines are established for setting the salary.



A person may be employed as a doctoral student for a maximum of eight years, but no longer than the equivalent of four years of full-time postgraduate research study.



All applications must be in writing and should include the following:



completed application forms for admission to postgraduate studies, and employment as doctoral student (forms available on the faculty website www.jur.uu.se/ under “Research education”),



a signed and witnessed curriculum vitae,



certified copies of degrees obtained and other relevant documents,



a description of the doctoral project with a time schedule for the entire period of study, and

a substantial piece of written work e.g. undergraduate degree final essay (or similar),



all documents attached to the application should be translated into English or Swedish.



Further information may be obtained from Torbjörn Ingvarsson, Director of Studies, phone: +46 18-471 2019, e-mail: Torbjorn.Ingvarsson@jur.uu.se or Christina Andersson, phone: +46 18-471 2054, e-mail: Christina.Andersson@jur.uu.se Union representatives are: Anders Grundström, Saco Council, phone: +46 18-471 5380, Carin Söderhäll, TCO/ST, phone: +46 18-471 1996, and Stefan Djurström +46 18-471 3315.



The application should be sent , preferrably by e-mail to: registrator@uu.se, or by fax + 46 18 471 2000, or by mail to:

Registrar´s Office,

Uppsala University,

Box 256, SE-751 05

UPPSALA, Sweden.





In any correspondence, please use the reference number UFV-PA 2010/2817.



Application deadline on 1 March 2011.





SOURCE: CLICK HERE

Wednesday, March 2, 2011

Full scholarship for Commonwealth nationals for MSc in Climate Change & DevelopmentPosted by Kitogo on March 2, 2011 at 3:12pm

.Full scholarship for MSc in Climate Change and Development at University of Sussex/Institute for Development Studies, UK

A full scholarship (fees plus maintenance and travel) funded through the Commonwealth Shared Scholarship scheme is available for applicants to the MSc in Climate Change and Development programme for entry October 2011.



Note: Potential applicants must undertake the following process in the order stated.



1. Check their eligibility for the award (see criteria below)



2. Submit an application for the MSc in Climate Change and Development using the online application facility at http://www.sussex.ac.uk/study/pg/2011/taught/3331/23691



3. Only after applicants have received an offer of a place on the course should they request an application form for the scholarship, be contacting climate@sussex.ac.uk. The deadline for applications for the scholarship is 1st May 2011.



Scholarship Criteria



Applicants must

(i) be nationals of (or permanently domiciled in) a Commonwealth developing country, and not currently be living or studying in a developed country (please see the booklet for a list of eligible countries)

(ii) hold a first degree at either first or upper second class level;

(iii) be sufficiently fluent in English to pursue the course

(iv) have not previously studied for one year or more in a developed country

(v) not be employed by a government department (for this purpose the Commission counts this as being employed by a Government Ministry).

(vi) be able to confirm in writing that neither they or their families would otherwise be able to pay for the proposed course of study

(vii) be willing to confirm that they will return to their home country as soon as their period of study is complete





Further information



(i) MSc in Climate Change and Development



This is unique course that aims to provide state-of-the-art training for the rapidly expanding market for development professionals with specialisation in climate change. The programme is strongly multidisciplinary and students will acquire specialist knowledge of the causes of climate change, the implications for developing countries, and the policy and practice of efforts to mitigate and adapt to a changing climate. Courses are taught by leading researchers in these fields from the world renowned Institute for Development Studies (IDS), the Geography Department and Science and Technology Policy Research Unit (SPRU).



a href="http://www.sussex.ac.uk/study/pg/2011/taught/3331/23691">http://www.sussex.ac.uk/study/pg/2011/taught/3331/23691>;

a href="http://www.sussex.ac.uk/climatechange">www.sussex.ac.uk/climatechange>;

Tel: +44 (0)1273 877686

Email: climate@sussex.ac.uk



(ii) Commonwealth Shared Scholarship



For full details of the Commonwealth Shared Scholarship scheme see http://www.cscuk.org.uk/docs/DFIDSSSBOOKLET2011vi.pdf

CONSERVATION RESEARCH FOR EAST AFRICA’S THREATENED ECOSYSTEMS (CREATE)

Kwa wale wanahitaji pesa ya field ya research hii inafaa sana.Hata kama umeanza field work waandikie uulizie kufuatana na area yako.Wanasponsor both Social siences and Conservation aspects.


The European Union has funded Frankfurt Zoological Society (FZS) to conduct a number of research projects between 2011 and 2015 (5 year funding period). Many of the projects call for expertise in both conservation and social science. Research will be conducted by graduate students under the supervision of affiliated faculty, FZS staff, and students’ own advisors. A list of project desc-riptions is appended; some project modifications may be possible to meet the needs of doctoral programs.









Funding is available for graduate students currently enrolled in a doctoral or master’s program. Funding for research expenses on CREATE projects including field work expenses, a small research award and student stipend for 6 to 12 months is available. Some students may be eligible for additional funding. There is a preference for East Africans and Swahili speakers but any interested graduate students or persons entering graduate school may send a CV and letter indicating their interest (see below). Evaluation of applicants will begin in February 20th, 2011 but applications will continue to be accepted until the positions have been filled.



Longer desc-riptions and application requirements are available from the CREATE website .

Please send any questions to: CREATE@fzs.org









Overview



The CREATE program will investigate key questions on the inter-relationships between poverty reduction, human health, resiliency to shocks and environmental conservation within two ecosystems: Serengeti in Tanzania and North Luangwa in Zambia. Applied research programs conducted in two distinct ecosystems will allow comparisons of the effect on factors such as capacity for local governance, local livelihood activities, landscape type and poverty. Moreover, south-south partnerships across the two ecosystems will help to identify and scale up best practices and maximize their impact on reducing poverty, improving human health and increasing resilience to disasters, while reducing direct and indirect threats to the two ecosystems.



The goals of the projects are to (1) improve understanding of the links between poverty, human health, disaster management and environmental sustainability while (2) actively informing local and international decision-making and policy development in two key African ecosystems.









CREATE builds on previous work of FZS which piloted the Convention on Biodiversity’s “Ecosystem Approach” to conservation in Serengeti and North Luangwa ecosystems. This approach is based on the perceived link between local poverty by communities living within ecosystems with high biodiversity and important ecosystem services. The goal was to conserve biodiversity through programs designed to improve livelihoods and reduce poverty.









Case Study 1: Impact of population growth on environment, resiliency to shocks and human health (Tanzania). This case study will examine the effects of community-level interactive service provision by trusted community health workers on human fertility and resource use in Tanzania. We will use this case study to provide data on the potential impact of improving resiliency and human health and reducing negative impacts on the environment through a cost-effective and direct measure of addressing human population growth.



Case Study 2: Income diversification through microcredit enterprises and the impact on poverty reduction, natural resource use and resiliency to shocks (Tanzania). Through a previous project, FZS established a sustainable microcredit approach to environmentally-friendly livelihood diversification. Self-generating micro-credit groups established in Serengeti specifically targeted former bushmeat hunters as a means of providing alternative income generation opportunities. This case study will investigate how diversification of livelihoods can contribute to poverty reduction and reduce dependency on natural resources.









Case Study 3: Examining information dissemination and informed decision-making (Tanzania and Zambia)

PART A: Tanzania. Pastoral communities around Serengeti National Park valued natural forests on village land more after seeing that effects of a recent drought resulted in fewer livestock losses in those areas with intact forest. This case study will examine (i) how information on natural resource use and resiliency to shocks inform household level perceptions about natural resource use, and (ii) the effect of this information on natural resource management

PART B: Zambia. Harvesting of edible caterpillars by rural households contributes to food security in North Luangwa Ecosystem, Zambia. Sustainable harvests depends on: (i) a healthy survivor population of caterpillars, (ii) availability of preferred tree species, and (iii) control of bush fires during the egg-laying period. This case study will examine linkages between harvesting methods and fire management, poverty alleviation, and resource management at household and community levels. Monitoring will enable evaluation of the impact of these feedback systems on natural resource management decisions.









Case Study 4: The role of improving food security on human health and natural resource use (Tanzania and Zambia). Both bushmeat and chickens provide a source of protein to households throughout Western Serengeti and North Luangwa; chickens are also an important source of supplemental income in hard times. Unfortunately poultry production in Tanzania and Zambia is severely limited by endemic poultry diseases and loss to wildlife. This case study will examine the impact of improved husbandry and poultry health practices on food security and household consumption of bushmeat.









Case Study 5: The role of information dissemination in reducing the costs of living with wildlife and improving household food security and resilience to shocks through decreased human-wildlife conflict (Zambia). Human-wildlife conflict in communities with high wildlife density has adverse effects on both household food security and wildlife conservation. This case study will use the existing human-elephant conflict trial-site to examine the relationship between the efficacy of conflict mitigation measures and the uptake rate of these measures by households and community institutions.



Justin J. Hokororo,



Programme Accountant



Frankfurt Zoological Society