Pages

Wednesday, October 20, 2010

tunachangia CCM bila ridhaa yetu wenyewe

Wadau,


Staki kuthibitisha haya maneno hapo chini kama ni kweli au si kweli,

kwani kipindi hiki mambo mengi yanajitokeza.

Kinachonisikitisha naamini usajili tuliofanyiwa wa simu zetu ulikuwa

ni uhuni mkubwa, kwani sasa hivi unaweza ukapata ujumbe hususan toka

CCM (nasikia hata CHADEMA), ukikuomba kuchangia au kueleza mafanikio

ya CCM, kitu kinacholeta picha kuwa namba zetu zinatumika kisiasa

bila ridhaa yetu.



"Kila Mtanzania anayepiga simu mtandao wowote, asilimia kumi (10%) ya

huo muda wa maongezi, fedha hizo zinaenda kuchangia Kampeni za CCM.

Kudhihirisha hili, mtu yeyote mwenye simu, chukua simu yako, nenda

kwenye sehumu ya kuandika ujumbe mfupi (SMS); kisha andika neno

"HAPANA" na tuma ujumbe huo kwenda namba "15016." Utapokea ujumbe huu

“Asante kwa ujumbe wako, utatolewa kwenye huduma hii ya changia

ushinde na CCM.”Hii ni hujuma tunayofanyiwa watumiaji wa huduma za

mawasiliano bila ridhaa yetu au kujulishwa hivyo na Mamlaka ya

Mawasiliano Tanzania (TCRA).



Kesho yake, October 14,2010, nadhani baada ya wahusika kushtukia idadi

ya watu watu wanaojiondoa kwenye huduma hii; na nilipokuwa najiondoa

kwenye hujuma hii kwa kutumia lini yangu ya Zain & Zantel, nilipokea

ujumbe huu “Asante kwa ujembe wako kama umeshiriki Changia ushinde

utaondolewa kwenye huduma. Kumbuka hakuna malipo kutumia mtandao wa

mawasiliano wa CCM.” Ujumbe huu wa pili nauona kama ujanja wa

kuwapumbaza watu kwani mantiki yake imevurugwa kwa maksudi. Hata hivyo

cha msingi hapa tusiangalie nyuma, tumeshahujumiwa, dawa ni kujiondoa

maana kujiondoa kwenye hujuma hii ni bure. Mjulishe ndugu na rafiki

yako tafadhali. "



Noel

No comments: